<p style="text-align:justify"><br />
<span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">TUME ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), imeto elimu kwa wananchi zaidi ya Milioni 2 katika mkoa wa Pwani, Lindi na Mtwara inayohusu Sheria ya makosa ya kimtandao, maadili na ulinzi wa mtoto dhidi ya makosa hayo.</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">Mwanasheria wa Tume hiyo, Vicky Mbunde, akizungumza kwa nyakati tofauti Kibaha mkoani Pwani Aprili 24, 2025 wakati akitoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Walimu cha A3, Uuguzi na Uandishi wa Habari pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Nyumbu aliwataka kuwa mabalozi na walinzi wa mtoto dhidi ya makosa ya kimtandao huku wakijiepusha kufanya makosa hayo.</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">Alisema makosa ya kimtandao yamekuwa yakitumika kwa kutumia vifaa vya kielektroniki kama kompyuta, simu janja na vishikwambi na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">"Makosa hayo ni kurekodi picha mbaya za watoto kama za utupu, kufanyiwa vitendo vya ukatili, kudhalilishwa na vitendo vingine vinavyofanana na hivyo na kuzisambaza mtandaoni," alisema Mbunde.</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">Mbunde alisema mwanafunzi yeyote atakapoona vitendo hivyo vikifanyika au anafanyiwa atoe taarifa kwa walimu, wazazi na polisi ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">Alisema vitendo hivyo havikubaliki katika jamii na ndio maana zimetungwa sheria kali dhidi ya mtu yeyote atakayebainika kutenda makosa hayo.</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">Wakili Baraka Chipamba kutoka tume hiyo alisema makosa yote hayo yakiwepo ya ubakaji, kutia mimba na utoaji wa mimba adhabu yake ni kifungo cha zaidi ya miaka mitano nafaini kuanzia shilingi milioni tano hadi milioni 20 au zote kwa pamoja.</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">Walimu wa shule hizo waliipongeza tume hiyo kwakutoa elimu hiyo na wakaomba iwe endelevu kwani itasaidia kuwaondolea watoto hao madhira ambayo yanaweza kuyapata kutokana na vitendo hivyo.</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">Tume hiyo inatoa elimu hiyo chini ya Kaulimbiu isemayo Mabadiliko ya Sheria ni fursa ya kujenga taifa lenye haki na usawa kwa wote</span></span></span></span></span></span></p>
<p style="text-align:justify"><span style="font-size:13px"><span style="color:#000000"><span style="font-family:Arimo,"Open sans",Helvetica,Arial,sans-serif"><span style="background-color:#ffffff"><span style="font-size:medium"><span style="font-family:arial">Kuhusu Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ni idara ya Serikali inayojitegemea chini ya Wizara ya Katiba na Sheria ambayo imeanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania, Sura ya 171, na ilianza kazi rasmi tarehe 21 Oktoba, 1983. Kwa mujibu wa sheria, Tume ina jukumu la kufanya mapitio ya sheria zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili ziandane na mazingira ya wakati uliopo kwa maendeleo endelevu</span></span></span></span></span></span></p>