Government Logo
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania

Ununuzi na Ugavi
  Majukumu ya Kitengo cha Ugavi na Ununuzi Mkuu wa Kitengo - Nessy E. Kyejo Kusimamia ununuzi wowote na uuzaji wa mali za Wizara kwa njia ya Zabuni isipokuwa usuluhishi na kutunuku zabuni ; Kuratibu shughuli za Bodi ya Zabuni ya Wizara; Kutekeleza maamuzi ya Bodi ya Zabuni ya Wizara; Kufanya kazi kama Sekritarieti ya Bodi ya Zabuni ya Wizara Kuandaa mpango wa Ununuzi na Uuzaji wa mali za Wizara kwa njia ya Zabuni; Kupendekeza ununuzi na uondoshaji wa mali za Wizara kwa utaratibu wa zabuni; Kukagua na kuainisha upungufu wa mahitaji katika Wizara na kutoa tamko kuhusu mahitaji hayo; Kuandaa nyaraka za zabuni kwa ajili wazabuni kushiriki; Kuandaa matangozo ya fursa za zabuni; Kuandaa rasmu za Mikataba; Kutoa mikataba iliyothibitishwa na kusainiwa; Kuandaa na kuhifadhi kumbukumbu za mchakato wa ununuzi na uuzaji wa mali za Wizara; Kuandaa na kutunza orodha au kitabu cha mikataba yote ambayo Wizara imetunuku; Kuandaa taarifa za kila mwezi kwa ajili ya Bodi ya Zabuni ya Wizara; Kuandaa taarifa ya kila robo ya mwaka juu ya utekelezaji wa mpango wa ununuzi na kuwasilisha katika kikao cha menejimenti ya Wizara; Kuratibu kazi za ununuzi na uondoshaji wa mali za serikali katika Idara na vitengo vyote vya Wizara; na Kuandaa taarifa nyinginezo kadri zitakavyo hitajika muda wowote.